Sifa 15 Za Mwanaume Mwenye Future Na Anayejitambua….☟😎 Thread -🧵👇


twitter thread from




Hizi hapa ni sifa 15 ambazo mwanaume mwenye future na anayejitambua lazima awe nazo..☟
1. Husimama kama Mwanaume

Siku zote hujitahidi kuonesha kuwa yeye ni mwanaume na sio mvulana mkubwa.

2. Ana malengo yaliyo wazi

Anajua na kusimamia malengo yake, ngumu kumkuta akiishi bendera kufuata upepo. Na anapenda kile anachofanya.

3. Anajiamini Mno

Mwanaume anayejitambua anaamini anaweza kufanikisha chochote na kwanza kila muda anapaswa kujifunza mambo mapya kwa ajiri ya ukuaji wake.

4. Anasapoti Wengine

Husaidia wengine kukua na wala hawezi kuwashusha ili yeye apande. Hawezi kuchukia wale anaowasaidia wakimpita kimaendeleo kwani anaamini mtoaji ni Mungu pekee

5. Husimamia Kauli zake

Haongei kitu ambacho hakimaanishi . Anaamini kuwa akiongea uongo ataharibu hadhi yake.

6. Mwenye Busara na Hekima

Ukiongea nae kila wakati unajifunza kitu, anakufanya ujisikie na ujiamini kuwa unaweza. Vijana wengi humuita rolimodo wao.

7. Kuwa Smart na Kunukia Vizuri

Haijlishi kazi au mazingira aliyopo, Atajitahidi awe smart na anukie vizuri no mara waaaaa…

8. Hatishwi na mafanikio ya wengine

Mwanaume imara, anayejiamini, anayejitambua na kuelewa wajibu wake, hatishwi na uimara wala mafanikio ya wengine.

9. Hukubari kukosolewa

Mwanaume anayejitambua atafurahi zaid pale anapokosolewa kuliko kusifiwa sifiwa hovyoo.

10. Hakimbii Matatizo

Hata kama tatizo ni kubwa namna gani hawezi kukimbia, atatafuta mbinu yoyote ya kulitatu hata kwa kushirikisha wengine.

11. Halii lii Hovyo.

Hata kama akifiwa au mahusiano yake yakivunjika, Humkuti akilia lia au kulalamika hovyo mbele za watu au mwenye mitandao ya kijamii.

12. Humjari Mpenzi wake

Hufanya kila njia mwanamke wake awe na furaha na amani na kumtimizia mahitaji yake yote.

13. Hawezi kucheat

Mwanaume anayejitambua hawezi kucheat, na hata ikitokea kwa bahati mbaya, hatokiri ili kulinda imani na amani ya mwanamke wake kwake.

14. Hana Mzaha

Sio mtu wa kupenda mzaha na wala sio mtu wa kuomba omba msamaha kila wakati isiyokuwa na kichwa wala mkia.

15. Mtu wa Watu

Mwanaume anayejitambua jamii yake humtambua kwa mchango wake. Hakosi kuhudhuria shughuli zote za kijamii labda awe na dharura. Ni mtu wa wapwa haswaa.

Hizo hapo ni baadhi tu ya Sifa za Mwanaume mwenye future na anayejitambua. Ukiwa na hizi sifa unaweza kuleta mabadiriko chanya kwako na kwa jamii nzima.
Kama umejifunza kitu kupitia #Uzi huu, ni muda wa kulipa fadhira kwa kufanya haya…☺☟

1. Nifollow @mchachu_ 💯

2. Retweet iwafikie wengi na usisahau kuweka notification on.

Weekend Njema❤

Leave a Reply

Your email address will not be published.